Lengo
na shughuli za kikundi chetu cha BAHATI ni kuinua hali ya
maisha
ya wanachama na familia zao.
Ili
kufika lengo la kikundi wanachama wa kikundi chetu watatekeleza shughuli
zifuatazo
Kushiriki kwenye mafunzo ya kujenga uwezo
·
Mafunzo ya uongozi na taratibu za kuendesha
benki kikundi
·
Mafunzo ya biashara (SPM)
·
Mafunzo ya Teknolojia rahisi
·
Mafunzo mengineyo
Kuendesha benki ya kikundi ili kuwawezesha wanachama kujiwekea
akiba (hisa) na kuchukua
Mikopo
yenye masharti nafuu.
Wanachama kuendesha miradi endelevu ya kiuchumi pamoja na
wanafamilia wao ili kuongeza
Kipato cha familia
Wanachama kusaidiana
kuendesha mradi wa pamoja kwa lengo la kutoa huduma muhimu kwa jamii na kujipatia kipato
No comments:
Post a Comment