Sunday 17 November 2013

UDHURU KATIKA VICOBA NI KUTOKUJITAMBUA

Mwanachama yeyote anayejiunga kwa ridhaa yake katika kikundi chochote kile kwa  manufaa yake na jamii nzima ni lazima ahudhurie kila kikao cha siku iliyopangwa na kikundi.
 
Ukiona mtu ana udhuru katika kikundi basi ujue huyo hajitambui na hatakuja kufanikiwa hata iweje, maana kama umeona kuna umuhimu wa kujiunga na wenzako ili muwe familia moja basi tambua huyo si familia, pia tambua kikundi ni sehemu ya kusaidiana, je utasaidiaje au kusaidiwaje ikiwa wewe udhuru kila kukicha, je kikundi kitakuwa na maendeleo gani ikiwa wewe una udhuru.  Mbaya zaidi siku unayofika katika kikao unawarudisha wanakikundi nyuma maana utaanza kuhoji maswali yasiyo na msingi wakati wenzako walishapita huko.
 
Nashauri wanavikundi mukutane wote kila kikao kwa siku iliyopangwa itokee bahati mbaya mwanakikundi awe na safari, amefiwa, au kuumwa.  Lakini kama unajitambua unaweza kutenga dakika 45 kila siku iliyopangwa ili kuhudhuria vikao.
 
"Wote tuna majukumu lakini kama yako yamezidi basi hufai kuwa katika kikundi"

Monday 11 November 2013

"Thinkers think and doers do. But until the thinkers do and the doers think, progress will be just another word in the already overburdened vocabulary of the talkers who talk."

Wanakikundi lazima tutambue kuna Thinkers na pia kuna Doers, yaani kuna wanaofikiri na wanaotenda je wewe uko upande upi?

Mfikiriaji au Mtendaji?

JINSI YA KUUNDA KIKUNDI CHA VICOBA

VICOBA (Village Community Bank) ni mfumo wa kuweka na kukopa kwa wanachama waliojiunga kwa pamoja na kuunda kikundi kwa malengo ya kujikwamua kiuchumi.

Mfumo huu ulianza Tanzania miaka kumi iliyopita na umeonyesha mafanikio makubwa kwa wanachama wake kuweza kukopeshana, kusaidiana katika matatizo mbalimbali, kuanzisha miradi ya pamoja ya kiuchumi.

MALENGO/MADHUMUNI YA KUUNDA VICOBA
Madhumuni ya kuunda vicoba ni kuunganisha nguvu na rasilimali za wanachama ili kuondoa umasikini na kuleta maendeleo kwa kufanya yafuatayo:-
  • Kuchangia/kununua hisa
  • Kuchangia mfuko wa jamii
  • Kuendesha mfuko wa kuweka na kukopa
  • Kushiriki katika mafunzo ya kuongeza ujuzi wa biashara, uongozi na uanzishaji wa shughuli mbalimbali za pamoja za maendeleo.
  • Kutafuata soko la pamoja na la uhakika kwa bidhaa za wanakikundi 

Kuna tofauti gani kati ya VICOBA na SACCOS?



VICOBA na SACCOS ni vikundi vya kiuchumi vyote vina malengo sawa isipokuwa mfumo wa uendeshaji.
  1.  Katika VICOBA wanachama uweka kiwango cha hisa na mara nyingi huanzia Sh.1000 na kuendelea, kiwango hicho ni kidogo ukilinganisha na kiwango cha hisa katika SACCOS.
  2.  WanaVICOBA umaliza mzunguko wao baada ya miezi kumi na mbili (12) na kufanya tathmini ikiwemo kugawana makusanyo na faida.
  3. Riba ya mkopo katika VICOBA ni ndogo (mara nyingi haizidi 10%)
  4. Kikundi cha VICOBA kinaundwa na wanachama 15-30, wanaoishi eneo moja au wanaofanya kazi pamoja.
  5.  Gharama za uendeshaji wa VICOBA ni ndogo kwani hakuna ofisi (wanachama huchagua mahali pa kukutana kwa muda usiozidi saa moja), vile vile viongozi wa VICOBA hawaajiriwi (wanafanya kazi za kujitolea)
VICOBA ikikuwa inaweza kuunda SACCOS. Mfumo wa Vicoba ni mzuri hasa kwa falsafa ya kuanza kidogo ili kuwa na kitu kikubwa hapo baadae. Licha ya kujihusisha na shughuri za kuweka na kukopa, wanavicoba husaidiana katika matatizo mbalimbali kama msiba na ugonjwa. Vile vile wanavicoba wanaweza kuanzisha mradi wa pamoja wa kikundi kwa kuunganisha rasirimali ndogo walizonazo. 
Hatua za Kuunda kikundi cha VICOBA
  1. Watu wenye wazo la kuanzisha kikundi kukutana (watu hao wasipungue kumi na tano na wasizidi thelathini)
  2. Wanachama kukusanya fedha za kiingilio (mara nyingi ni Sh. 10,000) kwa mwanachama. Fedha hiyo hutumika kununua vifaa kama leja,kasiki n.k. Fedha ya kiingilio vilevile hutumika kugharamia mafunzo ya awali na gharama ya usajili wa kikundi)
  3. Wanachama kuanza mafunzo yatakayosimamiwa na mwalimu mtaalamu wa mfumo huu wa vicoba.
  4. Wanachama kutunga katiba na sheria zitakayojumuisha kiwango cha hisa, mfuko wa jamii, siku ya kukutana n.k

Vicoba husajiliwa Brela kama jina la biashara (Business name) na kutambuliwa na halmashauri ya manispaa husika kupitia ofisi ya maendeleo ya jamii.
Mfumo huu ni rahisi kuuendesha na unamanufaa makubwa katika maendeleo ya kiuchumi. Ni fursa kwa vijana wenye mitaji midogo kuanzisha vikundi hivi ili kuunganisha rasirimali ndogo walizonazo na kwa pamoja kujiletea maendeleo.

Elimu ya Ujasiriamali ni Lazima kwa VICOBA

Imebainishwa kuwa vikundi vingi vya vicoba nchini licha ya kukabiliwa na changamoto ya mtaji vinahitaji elimu ya ujasiriamali ili Kuweza kufahamu jinsi ya kufanya biashara kwa faida badala ya kufanya biashara kwa mazoea jambo linalofanya vikundi vingi Kufilisika na kushindwa kuendelea.

KIKUNDI LAZIMA KIBUNI MIRADI MIKUBWA YA KATI NA MIDOGO

Kuna aina nyingi za miradi

Ipo miradi Mikubwa

Ipo miradi ya Kati

Ipo miradi Midogo

Kikundi kinatakiwa kufanya mambo haya na siku vinginevyo, la sivyo haina haja ya kuwa na kikundi

Sunday 10 November 2013

Lazima Tuelewe

wanakikundi ni lazima tuelewe wiki ya 14 hii, tujifunze kazi za mkutano mkuu unaofanyika maramoja kwa maka ambao ndio unachagua viongozi.

Tujifunze jinsi ya kutatua migigoro itakapojitokeza

Tujifunze jinsi ya kuweka akiba

Jinsi ya kusimamia mikopo ya wanachama

Tujifunze jinsi ya namna ya kutunga kanuni na taratibu za vikundi na kuandika michanganuo rahisi ya biashara, ambayo ni msaada mkubwa katika kupanua wigo wa biashara zetu.

Kimsingi hatutakiwi kuvunja kikundi mwisho wa mwaka bali tuanzishe miradi ya vikundi ambayo itashirikisha wanachama wote.

Lazima kikundi chetu kitambulike serikali za mtaa pamoja na majirani

Lengo linguine ni kupeleka ujumbe kwa wananchi kwamba VICOBA kama wengine wanavyodhani kimakosa kuwa ni vikundi vya kufa na kuzikana.  Wananchi wanakumbushwa kwamba hivi ni vikundi vya maendeleo ya uchumi.

Pia tujipange kualika vikundi mia tatu kuzindua kundi letu la BAHATI VICOBA
 hapa tutapata kiasi cha shilingi milioni tisa (9,000,000/=) za kuzindilia kikundi


BAHATI VICOBA kina bahati kama jina lake, kuna THINKERS ila kuna watu wanataka kuharibu kundi kama tutaendelea kupanga mikakati ya kibwege nje ya mikutano na kulalama nje ya vikao halali kundi hili litakuwa HOPELESS na hakuna maendeleo yatakayofikiwa.  wanajulikana waharibifu wa kikundi ila ipo siku watatajwa na wataachiwa kundi na wenye akili watatoka

VICOBA SI VIKUNDI VYA KUSAIDIANA WAKATI WA KUFA AU KUUMWA

VICOBA ni

BONYEZA HAPA:

http://www.habarileo.co.tz/index.php/makala/15221-vicoba-si-vikundi-vya-kufa-na-kuzikana-bali-vya-kiuchumi