Sunday 17 November 2013

UDHURU KATIKA VICOBA NI KUTOKUJITAMBUA

Mwanachama yeyote anayejiunga kwa ridhaa yake katika kikundi chochote kile kwa  manufaa yake na jamii nzima ni lazima ahudhurie kila kikao cha siku iliyopangwa na kikundi.
 
Ukiona mtu ana udhuru katika kikundi basi ujue huyo hajitambui na hatakuja kufanikiwa hata iweje, maana kama umeona kuna umuhimu wa kujiunga na wenzako ili muwe familia moja basi tambua huyo si familia, pia tambua kikundi ni sehemu ya kusaidiana, je utasaidiaje au kusaidiwaje ikiwa wewe udhuru kila kukicha, je kikundi kitakuwa na maendeleo gani ikiwa wewe una udhuru.  Mbaya zaidi siku unayofika katika kikao unawarudisha wanakikundi nyuma maana utaanza kuhoji maswali yasiyo na msingi wakati wenzako walishapita huko.
 
Nashauri wanavikundi mukutane wote kila kikao kwa siku iliyopangwa itokee bahati mbaya mwanakikundi awe na safari, amefiwa, au kuumwa.  Lakini kama unajitambua unaweza kutenga dakika 45 kila siku iliyopangwa ili kuhudhuria vikao.
 
"Wote tuna majukumu lakini kama yako yamezidi basi hufai kuwa katika kikundi"

Monday 11 November 2013

"Thinkers think and doers do. But until the thinkers do and the doers think, progress will be just another word in the already overburdened vocabulary of the talkers who talk."

Wanakikundi lazima tutambue kuna Thinkers na pia kuna Doers, yaani kuna wanaofikiri na wanaotenda je wewe uko upande upi?

Mfikiriaji au Mtendaji?

JINSI YA KUUNDA KIKUNDI CHA VICOBA

VICOBA (Village Community Bank) ni mfumo wa kuweka na kukopa kwa wanachama waliojiunga kwa pamoja na kuunda kikundi kwa malengo ya kujikwamua kiuchumi.

Mfumo huu ulianza Tanzania miaka kumi iliyopita na umeonyesha mafanikio makubwa kwa wanachama wake kuweza kukopeshana, kusaidiana katika matatizo mbalimbali, kuanzisha miradi ya pamoja ya kiuchumi.

MALENGO/MADHUMUNI YA KUUNDA VICOBA
Madhumuni ya kuunda vicoba ni kuunganisha nguvu na rasilimali za wanachama ili kuondoa umasikini na kuleta maendeleo kwa kufanya yafuatayo:-
  • Kuchangia/kununua hisa
  • Kuchangia mfuko wa jamii
  • Kuendesha mfuko wa kuweka na kukopa
  • Kushiriki katika mafunzo ya kuongeza ujuzi wa biashara, uongozi na uanzishaji wa shughuli mbalimbali za pamoja za maendeleo.
  • Kutafuata soko la pamoja na la uhakika kwa bidhaa za wanakikundi 

Kuna tofauti gani kati ya VICOBA na SACCOS?



VICOBA na SACCOS ni vikundi vya kiuchumi vyote vina malengo sawa isipokuwa mfumo wa uendeshaji.
  1.  Katika VICOBA wanachama uweka kiwango cha hisa na mara nyingi huanzia Sh.1000 na kuendelea, kiwango hicho ni kidogo ukilinganisha na kiwango cha hisa katika SACCOS.
  2.  WanaVICOBA umaliza mzunguko wao baada ya miezi kumi na mbili (12) na kufanya tathmini ikiwemo kugawana makusanyo na faida.
  3. Riba ya mkopo katika VICOBA ni ndogo (mara nyingi haizidi 10%)
  4. Kikundi cha VICOBA kinaundwa na wanachama 15-30, wanaoishi eneo moja au wanaofanya kazi pamoja.
  5.  Gharama za uendeshaji wa VICOBA ni ndogo kwani hakuna ofisi (wanachama huchagua mahali pa kukutana kwa muda usiozidi saa moja), vile vile viongozi wa VICOBA hawaajiriwi (wanafanya kazi za kujitolea)
VICOBA ikikuwa inaweza kuunda SACCOS. Mfumo wa Vicoba ni mzuri hasa kwa falsafa ya kuanza kidogo ili kuwa na kitu kikubwa hapo baadae. Licha ya kujihusisha na shughuri za kuweka na kukopa, wanavicoba husaidiana katika matatizo mbalimbali kama msiba na ugonjwa. Vile vile wanavicoba wanaweza kuanzisha mradi wa pamoja wa kikundi kwa kuunganisha rasirimali ndogo walizonazo. 
Hatua za Kuunda kikundi cha VICOBA
  1. Watu wenye wazo la kuanzisha kikundi kukutana (watu hao wasipungue kumi na tano na wasizidi thelathini)
  2. Wanachama kukusanya fedha za kiingilio (mara nyingi ni Sh. 10,000) kwa mwanachama. Fedha hiyo hutumika kununua vifaa kama leja,kasiki n.k. Fedha ya kiingilio vilevile hutumika kugharamia mafunzo ya awali na gharama ya usajili wa kikundi)
  3. Wanachama kuanza mafunzo yatakayosimamiwa na mwalimu mtaalamu wa mfumo huu wa vicoba.
  4. Wanachama kutunga katiba na sheria zitakayojumuisha kiwango cha hisa, mfuko wa jamii, siku ya kukutana n.k

Vicoba husajiliwa Brela kama jina la biashara (Business name) na kutambuliwa na halmashauri ya manispaa husika kupitia ofisi ya maendeleo ya jamii.
Mfumo huu ni rahisi kuuendesha na unamanufaa makubwa katika maendeleo ya kiuchumi. Ni fursa kwa vijana wenye mitaji midogo kuanzisha vikundi hivi ili kuunganisha rasirimali ndogo walizonazo na kwa pamoja kujiletea maendeleo.

Elimu ya Ujasiriamali ni Lazima kwa VICOBA

Imebainishwa kuwa vikundi vingi vya vicoba nchini licha ya kukabiliwa na changamoto ya mtaji vinahitaji elimu ya ujasiriamali ili Kuweza kufahamu jinsi ya kufanya biashara kwa faida badala ya kufanya biashara kwa mazoea jambo linalofanya vikundi vingi Kufilisika na kushindwa kuendelea.

KIKUNDI LAZIMA KIBUNI MIRADI MIKUBWA YA KATI NA MIDOGO

Kuna aina nyingi za miradi

Ipo miradi Mikubwa

Ipo miradi ya Kati

Ipo miradi Midogo

Kikundi kinatakiwa kufanya mambo haya na siku vinginevyo, la sivyo haina haja ya kuwa na kikundi

Sunday 10 November 2013

Lazima Tuelewe

wanakikundi ni lazima tuelewe wiki ya 14 hii, tujifunze kazi za mkutano mkuu unaofanyika maramoja kwa maka ambao ndio unachagua viongozi.

Tujifunze jinsi ya kutatua migigoro itakapojitokeza

Tujifunze jinsi ya kuweka akiba

Jinsi ya kusimamia mikopo ya wanachama

Tujifunze jinsi ya namna ya kutunga kanuni na taratibu za vikundi na kuandika michanganuo rahisi ya biashara, ambayo ni msaada mkubwa katika kupanua wigo wa biashara zetu.

Kimsingi hatutakiwi kuvunja kikundi mwisho wa mwaka bali tuanzishe miradi ya vikundi ambayo itashirikisha wanachama wote.

Lazima kikundi chetu kitambulike serikali za mtaa pamoja na majirani

Lengo linguine ni kupeleka ujumbe kwa wananchi kwamba VICOBA kama wengine wanavyodhani kimakosa kuwa ni vikundi vya kufa na kuzikana.  Wananchi wanakumbushwa kwamba hivi ni vikundi vya maendeleo ya uchumi.

Pia tujipange kualika vikundi mia tatu kuzindua kundi letu la BAHATI VICOBA
 hapa tutapata kiasi cha shilingi milioni tisa (9,000,000/=) za kuzindilia kikundi


BAHATI VICOBA kina bahati kama jina lake, kuna THINKERS ila kuna watu wanataka kuharibu kundi kama tutaendelea kupanga mikakati ya kibwege nje ya mikutano na kulalama nje ya vikao halali kundi hili litakuwa HOPELESS na hakuna maendeleo yatakayofikiwa.  wanajulikana waharibifu wa kikundi ila ipo siku watatajwa na wataachiwa kundi na wenye akili watatoka

VICOBA SI VIKUNDI VYA KUSAIDIANA WAKATI WA KUFA AU KUUMWA

VICOBA ni

BONYEZA HAPA:

http://www.habarileo.co.tz/index.php/makala/15221-vicoba-si-vikundi-vya-kufa-na-kuzikana-bali-vya-kiuchumi

VIONGOZI WA BAHATI VICOBA

MWENYEKITI
Saidi CHIMBIYANGU

KATIBU
Justine MADATI

MTUNZA HAZINA
Edna ROBERT

WAHESABU FEDHA
Robert MUJUNI
Anita BANA

WASHIKA FUNGUO
Fatuma MTENGULA
Mama BONGE
Mama NYALUSI

MTUNZA NIDHAMU
Mama CHIMBIYANGU


BIASHARA

Mchele:
Justine MADATI

Viti:
Juma MPIMBITA

MAKUSANYO YA FEDHA ZA VITI
Dada MLELWA

SUKARI
Justice MADATI

Biashara ya Mbogamboga



Biashara ya Upambaji



Biashara ya Mayai ya Kuku wa Kienyeji kwa Kikundi cha BAHATI VICOBA

BAHATI VICOBA UFUGAJI






Tunashauriwa kuwa na biashara ya ufugaji wa Mbuzi, Kuku na Ng'ombe pia uuzaji wa mayai

SIFA ZA KIONGOZI BORA

Kisaikolijia sifa za kiongozi ziko wazi na ni muhimu, mtu kuwa nazo kabla au baada ya kupewa cheo. Leo tunataka kuziangalia kwa undani sifa hizi, ili kama wananchi au viongozi wenye dhamana ya kuchagua watu wa kuongoza tuwatazame watu kwa sifa zao kabla na baada ya kuwapa nafasi. Sifa za kiongozi ni hizi zifuatazo:

 1. Awaze mafanikio makubwa
Kiongozi bora lazima awe na maono ya juu ya kuhakikisha kuwa nchi yake, kampuni yake sekta yake inapata mafanikio makubwa, hii ndiyo itakuwa dira ya kazi yake itakayompa muongozo wa kusimamia wafanyakazi na watendaji wote walio chini yake kufikia kiwango cha mafanikio anachokiwaza. Kiongozi asiyekuwa na mawazo ya juu ya kuendelea kutoka mahali alipo hafai.

 2. Awe na nia
Haitoshi kwa kiongozi kuwa na mawazo chanya peke yake bila kuwa na nia ya kuyatimiza. Hivyo, kiongozi atafaa kuchaguliwa kuwa kiongozi endapo tu atakuwa na uwezo wa kuratibu vema na kutekeleza alichowaza. Ajue njia anayopita, awatangulie anaowaongoza kwa vitendo.

 3. Ajitambue mwenyewe
Lazima kiongozi ajitambue mwenyewe ni mtu wa namna gani, ajue uwezo wake na upungufu wake na awe tayari kujiongezea maarifa kila siku, ili aweze kukabili changamoto na mabadiliko ya ulimwengu. Asome, afuatilie mambo yanavyokwenda na ajifunze kwa wenzake kuhusu kufanikisha malengo yake.

 4. Asimamie maamuzi
Kuna wakati malengo hukumbana na vikwazo, hivyo ni wajibu wa kiongozi kusimamia maamuzi sahihi na kuwa mtu wa mwisho. Kiongozi mwenye kubadilika badilika kama kinyonga, hafai kwa vile kukosa msimamo kuna maanisha udhaifu wa mipango na kujiamini.

 5. Adhibiti msongo wa mawazo
Tunamtarajia kiongozi mzuri awe ni mtu mwenye kupunguza msongo wa mawazo, ili kuifanya akili yake ifikie maamuzi sahihi, lakini kama atakuwa mwenye kuwaza mengi, atajikuta anachanganyikiwa na kuwa mtu wa jazba katika maamuzi na hivyo kuipotosha jamii.

 6. Akubali kukosolewa
Viongozi wasiokuwa na sifa za uongozi huwa hawakubali kukosolewa, wakidhani kuwa hiyo ndiyo njia ya kuthibitisha msimamo wao na usahihi wao. Kiongozi makini ni yule ambaye atakuwa tayari kukosolewa na kuwapongeza wanaomkosoa kwa kutazama mwenendo wake na usahihi wake. Asiyekubali kukosolewa hafai kuwa kiongozi.

 7. Awe msikilizaji
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kuwasilikiza watu walio chini yake, apokee maoni yao na ikiwezekana ayafanyie kazi. Lakini pia anatakiwa kuwafahamu kwa undani, ili aweze kuwaongoza vema kufuatana na hali zao. Akiwa na watu walemavu wenye kasoro kadhaa wa kadhaa anatakiwa kuwatambua kabla na baada ya kuwa kiongozi wao. Kuongoza usichokifahamu ni ujinga.

 8. Afuate haki
Kiongozi imara anatakiwa kufuata haki katika kuongoza kwake, asijione mwenye haki zaidi ya wale anaowaongoza katika sheria. Ni muhimu kwake kuwafanya walio chini yake kujiona wako huru katika mawazo na matendo. Kiongozi anayetumia nguvu na ukali kuongoza watu hafai. Hata yule mwenye kujivunia uongozi wake naye hafai.

 9. Awe egemeo la watu
Sifa nyingine ya kiongozi ni kuwa egemeo la watu wake katika shida na raha. Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa tayari kusikitika, kuomboleza, kufurahi pamoja na watu wa chini yake bila kujitenga nao. Ajitolee kuwatumikia watu kwa hali na mali na awe tayari kutumika zaidi kwa maslahi ya wengine.

 10. Atie moyo watu
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa na uwezo wa kuwatia moyo walio chini yake ili waweze kuendeleza vipaji vyao. Haipendezi kwa kiongozi kuwavunja moyo watu kwa kauli za kudharau kazi na jitihada zao walizojaribu kufanya katika kutekeleza majukumu yao kama wafanyakazi au wananchi.

 11. Afurahie mafanikio
Sifa nyingine muhimu ya kiongozi ni kuwa tayari kufurahia mafanikio aliyopata pamoja na watu wake. Ni wajibu wa kiongozi kutoa tuzo, kuwashukuru wafanyakazi wake na kuwa tayari kuwapa ofa. Hii itasaidia kuwafanya watu waone hawajapoteza nguvu zao katika utendaji wao na kwamba wanakubalika. Si busara wakati mwingine kuwakosoa watu mbele ya hadhara na kueleza kutofurahishwa na kazi zao.

 12. Aungane na wa chini yake
Mtu kuwa kiongozi haimaanishi amekuwa wa tofauti na watu wengine kiasi cha kushindwa kuchangamana nao kama wanavyofanya baadhi ya viongozi. Kiongozi mwema ni yule atakayeungana na watu wake katika maisha ya kawaida. Kuwa kiongozi haimaanishi kwamba watu watakufuata wewe kila siku, wakati mwingine wewe unatakiwa kuwafuata wao na kuwa nyuma yao hata mahali walipokosea au wanapokabiliwa na makosa, watetee na uoneshe kuwajali na kuwapigania, makosa utayahesabu baada ya utetezi wako kukamilika.

13. Akubali lawama
Kama kiongozi amefanya mambo ambayo jamii haikupendezwa nayo anachotakiwa kufanya ni kukubali kulaumiwa. Ikiwa anaongoza kitego cha umeme kwa mfano na watu hawakupata nishati hiyo kwa wakati hatakiwi kukwepa lawama, vivyo hivyo kwenye wizara na idara au nchi kwa ujumla.

14. Afahamu kutatua matatizo
Kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa na uwezo wa kuzuia migogoro na kuitatua kwa haraka. Muongozo mzuri katika eneo hili umesimama katika mawasiliano na watu wa chini, mawasiliano haya ndiyo yatakayomuwezesha kiongozi kujua matatizo waliyonayo wafanyakazi wake au hata jamii anayoiongoza na hivyo kumfanya apate wasaa wa kuyashughulikia mapema.

 15. Ajifunze kwa makosa
Wakati mwingine mawazo na mipango inaweza ikaenda kombo, hivyo ni wajibu wa kiongozi kujifunza kutokana na makosa yake au ya wale anaowaongoza, ili kuepuka kurudia makosa yale yale na kumfanya apoteze sifa za kuwa kiongozi mzuri.
Mwanafalsafa Winston Churchill aliwahi kusema "The price of greatness is responsibility." Thamani ya ukuu ni uwajibikaji.

 16. Awe mwaminifu
Miongoni mwa maeneo magumu kabisa yaliyowashinda na yanayoendelea kuwashinda viongozi wengi ni uaminifu. Kiongozi bora ni yule ambaye yuko tayari kusimamia muongozo wa katiba ya nchi au marufuku alizowekewa katika madaraka yake. Hii inakwenda sambamba na kutowaonea, kuwanyanyasa wa nchini yake kwa kutumia cheo chake.

 17. Awe mkweli
Viongozi wengi hasa wa kisiasa siku hizi ni waongo hakuna mfano, wamejaa ahadi zisizotekelezeka na hata wanapogundua kuwa hawana uwezo au wamekwama kuzitimiza, hawaoni haja ya kutubu mbele ya wanaowaongoza. Kiongozi makini ni yule atayekuwa tayari kuonesha ubora wa matendo na kauli zake.

 18. Asiwe mwenye majungu
Kuna baadhi ya viongozi kwenye maofisi wanaendekeza sana majungu na pengine kuyapa umuhimu wa hali ya juu. Hii ni sifa mbaya kwa kiongozi yo yote, hivyo anayetumikia ‘umbea’ katika ofisi aliyokabidhiwa kama mkuu anapaswa kuondolewa. Kiongozi makini atatumia uwezo wake kuzuia watu wasimsengenye/wasisengenyane kwa kuwa muwazi na mwenye kufungua milango ya watu kumuona na kumlaumu na kueleza hisia zao.

 19. Awe bora
Kwa kila analofanya kama kiongozi lazima alifanye kwa ubora, asiwe mtu mwenye kulipua kazi na kufanya chini ya kiwango cha uwezo wake. Kila siku katika kazi, maamuzi, usimamizi, utekelezaji lazima atumike zaidi ya uwezo wake.

KUTOKA KUAJIRIWA MPAKA KUJIAJIRI MAMBO 8 YA KUZINGATIA​.

Kuna sababu mbalimbali kwanini mtu atake kuajiri, badala ya kuajiriwa, mfano kipato kidogo anachopata katika kazi husika, hitaji la kutaka uhuru zaidi binafsi wa kufanya kazi, hitaji la kuweza kutoa ajira kwa wengine na zaidi sana kuweza kutumia vema kipaji na uwezo wa kuzalisha ambao katika kazi ya sasa mtu hapati nafasi ya kufanya hivyo.
Kujiajiri ni jambo linalohitaji maandalizi ya muda mrefu na kuna mambo ya msingi kuyafahamu, haiwezekani tuu , ukaacha kazi na kusema ok, acha nijiajiri.
Makala hii inachambua mambo ya msingi ya kujiandaa na kuyafahamu kabla mtu hajaamua kuacha kuajiriwa.

Mkakati ni muhimu: Wazo au ndoto isiyo na mkakati wa kuitimiza ni upuuzi yaani ndoto hiyo au wazo hilo halina maana, hivyo basi ndoto yako ya kujiajiri siku moja, ni lazima iwekewe mkakati wa kuifanikisha ikiwa ni pamoja na muda hasa wa lini utaitimiza hiyo ndoto.
Katika kuweka mkakati huu wa kutimiza ndoto yako, fanya utafiti wa kina kuhusu mipango yako binafsi ya maisha, mtazamo wako kuhusu maisha, mpenzi/mke wako, familia yako, na hali ya jamii kwa ujumla inavyoenda kama vile mabadiliko ya hali ya kisiasa, teknolojia, na uchumi.
Tengeneza malengo ya aina ya shughuli unayotaka kuifanya ukiacha kuajiriwa, na pima uwezekano wa shughuli hiyo kufanyika kweli na kama itakulipa. Utambue pia aina ya watu na rasilimali nyingine utakazozihitaji, na jinsi utakavyozipata.
Unahitaji fedha: Ndio, unahitaji kiasi cha fedha za kutosha kununua vifaa na malighafi za kutengenezea bidhaa yako. Pia unahitaji fedha za kuwalipa wafanyakazi wako, na zaidi sana , unahitaji fedha za kuendesha maisha yako na familia yako , kwa kipindi fulani kabla ya biashara kuanza kukulipa mshahara. Hivyo kabla haujaacha kibarua chako, hakikisha umetengeneza bajeti ya kutosha na una akiba ya kutimiza mahitaji ya bajeti yako. Usingependa uache kazi halafu uanze kuwa omba omba kwa rafiki na jamaa, au uanze kujuta.
Network ni muhimu: Kumbuka katika kujiajiri kwako, utahitaji wateja, washirika, wafanyakazi na hata washauri mbalimbali ili mambo yako yaende vizuri. Hivyo, wakati ukiwa umeajiriwa ndio wakati wako muafaka wa kutengeneza na kupanua wigo wako wa watu unaowafahamu na waliokaribu nawe.
Kumbuka kuendeleza mawasiliano kwani watu hawapendi kuona wewe unataka kuwatumia tuu kisha unawatupa. Endeleza mawasiliano walau hata kwa salamu tuu. Zaidi sana, heshimu watu wote, hata usiowafahamu au wale unaodhani 'sio watu muhimu'.
Jenga taswira nzuri kwa jamii kwa lugha fasaha, picha na matukio mengine, usifanye watu wakufikirie vibaya.
Usipitwe na wakati: Hakikisha kuwa unafuatilia taarifa za matukio, dili na watu wanaohusiana na aina ya shughuli unayopanga kuifanya wakati utakapojiajiri. Hii itakusaidia kupata uzoefu na kusoma alama za nyakati, na pengine kutambua fursa nyingine zaidi.
Endelea kujifunza zaidi kuhusu kazi yako, watu na jamii kwa ujumla kwani kujiajiri kunahitaji uzoefu zaidi, na zaidi sana uwezo wa kupambana na changamoto nyingi ambazo nyingine haujawahi kukutana nazo kabisa, ila taarifa za awali na kujua jinsi mambo yanavyoenda kwa ujumla katika jamii vitakufanya ushinde changamoto.
Maana halisi ya biashara: Baada ya kuacha kuajiriwa, hautarajii kuwa mtu wa ‘kuganga njaa’ yaani kufanya biashara ili mradi tuu hela iingie, lakini haujui mwelekeo wa biashara yako upoje, na wala hakuna mkakati wa kuikuza na kuimarisha biashara husika.
Biashara inahusu kutimiza mahitaji ya watu, kwahiyo ili mradi utakuwa na uwezo mkubwa wa kutimiza mahitaji ya watu, na kuendelea kuhamasisha watu zaidi kuja kwako uweze kutimiza mahitaji yao , basi biashara itakua, na itaendelea kuwa endelevu.
Kinyume cha hapo, ushindani utakutoa katika biashara kwani wateja watakambilia kwa wengine. Biashara sio tuu kupata wateja, ni vile kuweza kuendelea kupata wateja na kuendelea kupanua biashara.
Inabidi uipende shughuli husika unayoifanya, na uweze kutimiza mahitaji ya wateja kupitia biashara husika.
Muda wako mwingi utautumia katika shughuli yako mpya utakayojiajiri hivyo, kama ambavyo kazi uliyonayo pengine ‘inakuboa’, hakikisha ajira yako binafsi ‘haikuboi’.
Umuhimu wa wafanyakazi: Watendaji wa shughuli husika za biashara yako utakayoianzisha ni muhimu wawe wenye ujuzi na uzoefu wa kutosha wa kufanya shughuli husika, na uweke mikakati ya kuwapatia nyenzo zote muhimu za kufanyia kazi ikiwemo teknolojia na mazingira mazuri ya kazi. Hivyo basi wakati unajiandaa kujiajiri tilia maanani hili katika bajeti yako ya kuajiri. Usingependa wafanyakazi wao wajisikie vibaya kama vile wewe ulivyojisikia vibaya katika ajira yako fulani (pengine ajira yako ya sasa). Muda huu ambao umeajiriwa, ndio muda pia muafaka wa kusaka 'vipaji'- yaani watu ambao utafanya nao kazi utakapojiajiri.
Inakuhusu wewe : Mafanikio yako katika kujiajiri yanategemea mambo mengi ila zaidi sana yanakutegemea wewe. Je, nini hasa sababu yako ya kutaka kujiajiri?
Ni kweli una bidhaa au huduma haswa ya kupeleka sokoni itakayokufanya iendeshe maisha yako na kuiendeleza biashara husika au ni hasira tuu za jinsi bosi wako anavyokuchulia hapo ofisini kwako, au kwakuwa mshahara uliopo sasa haukutoshi. Je, mipango yako mingine ya maisha ipoje?
Ndoto zako za kusoma, au kuishi sehemu tofauti tofauti, pengine mkoa mwingine tofauti na uliopo sasa, au pengine hata nchi husika. Je, yote hayo yanaathiri vipi mipango na mikakati yako ya kujiajiri, bila kusahau msukumo toka kwa familia yako.
Ndoto sahihi: Ni kweli kuwa upo sahihi kufikiria au kuota kufanya biashara kubwa na yenye mafanikio sana, lakini kumbuka mafanikio hayaji kwa usiku mmoja, na hata kama yatakuja kwa usiku mmoja, inahitajika kazi ya muda mrefu kuyafanya yawe endelevu.
Hivyo basi, usingoje wakati ‘muafaka’ wa wewe kuwa na kiasi kikubwa cha fedha au kwamba ‘umeyaset’ vema mambo yote.
Anza kidogo kidogo, kubali kufanya makosa, na tambua kuwa hata kama utafanya uchambuzi na uchunguzi wa kutosha kuhusu soko, jamii na teknolojia, hali halisi unayoenda kukumbana nayo inaweza kuwa tofauti na ile uliyojifunza wakati wa uchambuzi au uchunguzi wako kwakuwa hicho unachoenda kufanya ni kipya hakikufanyiwa uchambuzi, bali unakifanya kutokana na uchambuzi uliofanya hapo awali.
Kuna mtu mwingine atakuja kutumia makosa au mafanikio yako kupanga mambo yake.

Hadi sasa BAHATI VICOBA imekopesha zaidi ya shilingi milioni nne (4,000,000/=)

Ndugu wanakikundi,

Tunafuraha kuwatangazia kuwa hadi sasa wiki ya 14 kikund chetu kimeanza kukopeshana na hadi sasa kikundi kimetoa mkopo wa shilingi milioni nne taslimu.

Umbeya, majungu, Kusengenya vinavuruga maendeleo

Wanakikundi wa Bahati VICOBA mnaaswa kuwa na ushirikiano na upendo katika kikundi chenu kama hamtaifuata salamu ya VICOBA basi mtabaki kunung'unika na kusengenya pembeni.  Wengi wenu hamna kazi za kufanya hivyo inawafanya kila muambiwalo la msingi mnahisi kuburuzwa ila tulizeni akili na mjue hamburuzwi ila hakuna maendeleo ya lelemama, kubalini fauateni maelekezo mnayopewa na wabunifu ili muje muone maendeleo.

Ndugu wanakikundi nayaongea haya kwa uchungu kwa kuwa naona kuna watu wasio waaminifu wanaanza kuvuruga kikundi, hakuna ubunifu, kuna majungu tu, kila tunalopanga mnalipeleka kwenye kundi linguine ni aibu sana mwanakikundi kunyenyekea kundi linguine kisa unapewa HISA na JAMII ni aibu sana kufuatilia fedha iliyo benki kama vile imeliwa hamtaendelea nawaambia.  Kama mnataka maendeleo fuateni mambo ya msingi na myafanyie kazi na si kukaa pembeni na kuanza kusimanga.

Sunday 11 August 2013

VIONGOZI WA HABATI GROUP

Viongozi hawa wamechaguliwa kwa mara ya pili baada ya kugawana Groups mbili.  Sababu ya kufanya uchaguzi tena ni kuwa wanachama walifika 46 hivyo ilibidi wanachama watengwe katika vikundi viwili, hivyo kikundi cha JUHUDI kiliundwa tena na wanachama wa mwanzo kumi na saba (17) ambapo kikundi cha BAHATI kilipunguzwa wanachama sita (6) na kupewa JUHUDI, na kuzaliwa kikundi cha pili ambacho ni BAHATI hivyo wanachama 23 kila upande waliunda vikundi.  Na hawa ni viongozi wa BAHATI Group;

MWENYEKITI
Bi. Magret Katundu

KATIBU
Bi. Alice Magesa

MWEKA HAZINA
Bi. Edna G. Robert

WASHIKA FUNGUO
Bi. Magdalena Shirima
Bi. Beatrice Kilimo
Bi. Fatuma Mtengula

WAHESABU FEDHA
Bi. Imakulata Onyango
Bi. Anitha Bana

WATUNZA NIDHAMU
Bi. Salome Chimbyangu
Bi. Donata Kindole

MAJINA YA WANAKIKUNDI BAADA YA KUTOKA VIKUNDI VIWILI JUHUDI NA BAHATI

NA HAYA NDIO MAJINA YA BAHATI GROUP

KUNDI LA I

1.   BI. EDNA G. ROBERT
2.   BI. ALICE MAGESA
3.   BI. BEATRICE KILIMO
4.   BI. CATHERINE KIRENGA
5.   BI. NICE MSHANA

KUNDI LA II

6.   BI. ANITHA BANA
7.   BI. MAGRETH C. KITUNDU
8.   BI. DONATHA KINDOLE
9.   BI. FATUMA MTENGULA
10. BW. JUMA MPIMBITA

KUNDI LA III

11. BW. JUMA MASHAKA
12. BI. IMAKULATA ONYANGO
13. BI. ELIZABETH CHRISTIAN
14. BW. ROBERT J. KADALLAH
15. BI. MAGDALENA SHIRIMA

KUNDI LA IV

16. BI. ANTIA RWEGASIRA
17. BI. SALOME CHIMBYANGU
18. BI. MARY TUNZO
19. BI. HINDU SENYANGE
20. BW. ROBERT  B. MUJUNI

KUNDI LA V

21. BW. HUSSEIN MOHAMED
22. BI. PHOIBE MSHANA
23. BW. MUTALEMWA T. MUJUNI

Monday 5 August 2013

PESCODE PICTURES AND EVENTS






















UPIMAJI WA KISUKARI KWA WANAKIKUNDI

Kutokana na mfumo wa maisha tunayoishi kwa sasa wanadamu, magonjwa yamezidi hasa kisukari.  Kikundi cha Bahati kimeona ni vyema kwa sana kwa wanakikundi kuanza kupima kipimo cha sukari.  Na imeshauriwa kila mwanakikundi alete watu wasiopungua 10 ili wapate huduma ya vipimo.

Sunday 4 August 2013

SIRI YA UTAJIRI



Siri moja wapo ya kuwa tajiri ni kujenga tabia ya kuweka akiba. Kwa wajasiriamali wadogo swala la kuweka pesa zao benki na kukopa huwa ni swala gumu hasa vijijini ambako hakuna huduma hiyo, kuna njia nyingine ambayo wataalamu wamebuni kuwawezesha kuitumia nayo ni  kuweka akiba zao kwenye VICOBA. Watu wengi wamekuwa wakijiuliza vicoba ni nini? Leo nitaelezea kuhusu historia ya mfumo wa VICOBA muundo, kanuni na taratibu za mfumo wa kuweka na kukopa vijijini  (Village Community Banks - VICOBA)


 Mfumo wa Kuweka na Kukopa Vijijini (Village Community Banks - VICOBA) ni mpya hapa nchini kwetu, mfumo huu uliingizwa nchini na Shirika la CARE International, Tanzania mwaka 2000. VICOBA imeenea katika sehemu nyingi Tanzania na idadi ya Wanachama wa VICOBA Tanzania inakadiriwa kuwa 25,542, hisa 25,542 zenye thamani ya Tshs. 2,298,780,000  vikundi 912 wastani wa wanachama 28 kila kikundi. Mikopo iliyotolewa ni Tshs. 3,065,040,000. Mfumo huu humilikiwa na wanachama wenyewe kwa njia ya kujitolea, kujenga uwezo wa mtaji, kubuni miradi ya kifamilia, kutumia vizuri mikopo. Mfumo huu ni rahisi kuendesha kwani unatumia kumbu kumbu rahisi kwa mazingira ya wanachama.  Huwawezesha wanachama kuweka akiba na kukopeshana bila kuomba msaada kwa wafadhili wala kukopa benki. Faida inayopatikana hugawiwa kwa wanachama kutokana na mchango wa kila mwanachama.  Mfumo wa VICOBA ni shirikishi unaojengwa katika msingi ya upendo, ushirikiano na kuaminiana miongoni mwa wanachama. Kutokana na sharti hili muhimu, mfumo huu unachangia kurekebisha  watu wenye tabia mbaya na wasiokubalika katika jamii na kuwafanya wawe raia wema, ili wakubalike kwenye vikundi na kudhaminiwa na wenzao. Mfumo huu unalenga katika kubadilisha taratibu mbaya (zisizoendelevu) za maisha ili kuziwezesha familia  kujiewekea malengo maalumu ya maisha na kuandaa na kuitekeleza mikakati ya kuyafikia malengo yao hatua kwa hatua. Hii ni pamoja na kuwa na matumizi mazuri ya fedha kutika familia, kujituma katika kufanya kazi.  Mfumo huu unaurahisi wa kupata mikopo ya masharti nafuu kijijini na husaidia kuwawezesha wanakijiji (wanachama) kujiwekea hisa kila wiki katika benki yao katika eneo husika na kwa kiwango kidogo kulingana na uwezo wao pasipo na gharama yoyote.

Huduma  zifuatazo hutolewa na Vicoba kama vile; uundaji wa Vikundi vya Kuweka na Kukopa Vijijini (VICOBA) kibenki kwa kujitolea, kuandaa vifaa vya kibenki na masomo ya kufundishia, kutoa mafunzo ya  uongozi wa vikundi na kuweka na kukopa. Kutoa mafunzo ya biashara yanayolenga katika kuwawezesha wanachama kuweza kuchagua miradi mizuri ya kiuchumi,teknolojia nyepesi, kuandaa mipango mizuri ya kuanzisha na kuendesha miradi yao na mbinu za kusimamaia miradi hiyo kwa faida. Kufanya utafiti wa masoko na kuandaa mikakati ya masoko, Kuendesha shughuli za kibenki na ushauri mkwa vikundi. Kusaidia vikundi kuratibu usambazaji wa pembejeo na raslimali zingine.

Muundo wa uongozi kikundi cha VICOBA huundwa na wajumbe tisa ambao huchaguliwa kidemokrasia kwa kuzingatia kazi za kila kiongozi na uwezo walionao. Miongoni mwa viongozi hawa ni: wajumbe watano wa Kamati Tendaji yaani Mwenyekiti, Katibu, Mweka Hazina, na wahesabuji fedha wawili. Kundi la pili ni la viongozi wa kikundi ni: washika funguo za sanduku la kikundi watatu na mtunza nidhamu wa kikundi. Viongozi hawa huchaguliwa kidemokrasia na wanachama wote kwa kuzingatia sifa walizonazo katika kuongoza kikundi. Viongozi hawa hubaki madarakani kwa mzunguko mmoja ambapo sawa na miezi 9 - au zaidi Mzunguko wa kikundi hufungwa kwa muda wa wiki moja (1) hadi tatu (3), mara nyingi hii, hufanywa wakati wa sherehe za kidini au za mwisho wa mwaka au wakati wa kazi nyingi za kilimo, ukame, au uhaba mkubwa wa chakula, maji nk. Hisa zote zinazopatikana hugawanywa kwa wanachama pamoja na faida ili kusaidia kulipia gharama mbalimbali za familia kama vile kilimo, kununua chakula, nguo, ada za shule za watoto, na kugharamia sherehe na matumizi mengine muhimu ya familia. Mzunguko hufungwa ili kutoa nafasi ya kutosha kwa wanachama kushiriki kikamilifu katika kutatua matatizo yanayozikabili familia zao kipindi hicho. Mzunguko mpya huanza mara ya muda uliopangwa kupumzika kwisha. Marekebisho mhimu ya sheria za kikundi, uongozi na taratibu za kuendesha mikutano ni muhimu kufanyika wakati wa kufunga mzunguko ili kuboresha ufanisi wa kikundi katika mzunguko unaofuata.
 
Shughuli zote za vikundi vya VICOBA huendeshwa na wanavikundi wenyewe kwa njia ya kujitolea. Uzoefu unaonyesha kuwa wanavikundi huweza kuendesha vizuri shughuli zao baada ya kupatiwa mafunzo haya ya uongozi na usimamizi wa kazi za vikundi kutoka kwa wataalamu wa mfumo wa VICOBA. Kazi/wajibu wa wanakikundi ni: - Kushiriki kwenye mikutano na mafunzo ya vikundi. - Kuweka hisa za kila wiki. - Kuendesha miradi ya kiuchumi. - Kuchukua mikopo na kurejesha. - Kuchangia mfuko wa jamii na bima ya mikopo. - Kushiriki kikamilifu katika kuendesha miradi ya pamoja ya kikundi Vikundi vya VICOBA huandaa mipango yao na kufanya maamuzi yote kwa njia ya vikao ; ambavyo ni mkutano wa kila wiki , Mkutano Mkuu maalumu na Mkutano Mkuu wa kawaida wa mwaka.

Kwa sasa vikundi hivi huendesha shughuli zao chini ya sheria ya sekta isiyo rasmi na kuendesha shughuli zake chini ya uangalizi/ ulezi wa serikali za mitaa au halmashauri za miji na wilaya husika. Vikundi vinavyofadhiliwa na mashirika hulelewa na kupatiwa msaada wa kitaalamu kupitia mashirika yao pamoja na ofisi za serikali za maeneo yao wanayohusika. Ili kuhakikisha taratibu zao zinafuatwa kikamilifu na wanachama wake ni muhimu vikundi kujitungia sheria ndogo ili kuthibiti ukiukaji wa taratibu zilizowekwa na kuhakikisha kwamba kila mmoja anawajibika ipasavyo.
 
Mafunzo ndio shughuli inayopewa kipaumbele zaidi katika mfumo huu wa VICOBA. Hii ni kwa sababu tafiti mbalimbali zilizofanyika zinaonyesha kuwa kukosekana kwa ujuzi au mbinu za kibiashara ndio kiini cha matatizo yanayozorotosha jitihada za kuleta maendeleo endelevu nchini hususani kwa wananchi waishio vijijini.

Mafunzo ya mfumo wa VICOBA yamegawanyika katika makundi makubwa matatu ambayo ni:- (a) Mafunzo ya uongozi wa kikundi na uendeshaji wa shughuli za kuweka na kukopa (b) Mafunzo ya mbinu za biashara ya  kuchagua, kupanga na kusimamia mradi wa ki-uchumi (c) Mafunzo ya teknolojia rahisi za kuboresha ujuzi wa uzalishaji wa bidhaa za wana-kikundi kama vile ufugaji wa nyuki, (Bee keeping) kilimo bora cha mbogamboga kazi za mikono, ufugaji kuku, mbuzi ng’ombe, kuuza mayai, kuchimba kisima cha maji, biashara ya usafirishaji,n.k Mafunzo haya hutolewa kabla ya wanachama wa kikundi kuchukua mkopo. Lengo la mafunzo haya ni kuwaandaa wana-kikundi kiujuzi na kuwawezesha, kubuni, miradi mizuri ya kiuchumi na kuandaa mipango ya namna nzuri ya kuendesha na kusimamia biashara hizo. Mafunzo ya Kuweka na Kukopa na yale ya mbinu za biashara hutolewa kwa kipindi 12 kila wiki wanakikundi hufundishwa kipindi kimoja. Wakati huu wa mafunzo pia huweka akiba zao kwa njia ya hisa ili kutunisha mfuko wao ambao baadaye hutumika kwa kukopeshana. Mafunzo ya teknolojia rahisi hutolewa kwa wana-kikundi wanaoiendesha miradi ya uzalishaji bidhaa mbalimbali kama vile kazi za mikono, ufugaji, kilimo cha mbogamboga na shughuli zingine zinazohitaji ubunifu na mafunzo maalumu. Mafunzo haya hutolewa ili kuongeza ubora wa bidhaa zinazozalishwa Uchangiaji wa gharama za mafunzo Kwa kawaida wanachama wa VICOBA hufundishwa mafunzo wanayotaka wao wenyewe. Vikundi vimeanzishiwa mfuko wa mafunzo ambao kila mwanachama huchangia kiasi kidogo cha fedha kwa ajili ya kuchangia gharama za mafunzo haya. Kutokana na uwezo mdogo wa wanavikundi, wafadhili mbalimbali ikiwemo Serikali na Mashirika yasiyo ya kiserikali yamekuwa yakijitokeza kuchangia gharama ya mafunzo haya. Mfano Mashirika ya CARE Tanzania, WCRP, WCST, WWF, Ofisi ya Makamu wa Rais, WWF Tanzania, ITECO Engineering, Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Uropean Union, shirika lisilo la kiserikali la LAMP, Orgut, FREBU CO. LTD, nk
 
Kulingana sheria mama za mfumo huu wa VICOBA, mwanachama anatakiwa kuweka hisa 1-3 kila wiki. Kiwango cha hisa huamuliwa na wanakikundi wenyewe. Hata hivyo, kulingana na thamani ya fedha yetu kiwango cha chini kinachoweza kumnufaisha mwanachama kwa sasa ni shilingi mia tano (500). Mwanachama anaruhusiwa kuweka hisa moja, mbili hadi tatu kila wiki ili kutunisha mfuko. Matumizi ya Hisa ya mwanachama Hisa ni muhimu zana kwa mwanachma kwa sababu zifuatazo: (i) Ni akiba ya mwanachama ambayo huichukua mwishoni mwa mzunguko pamoja na faida au wakati mwingine wowote apatapo matatizo kulingana sheria za kikundi chao. Kwa kawaida hisa zinazochukuliwa katikati ya mzunguko hutolewa bila faida (ii) Hisa hutumika kama kigezo cha kujua kiwango cha mkopo ambacho mwanachama wa kikundi anaweza kuomba kutoka  

kwenye benki yao. Mfumo wa VICOBA unamruhusu mwanachama kuchukua mkopo hadi mara tatu ya hisa alizoweka. Hata hivyo, uamuzi wa kupatiwa mkopo huo utazingatia matumizi na uhakika wa mwanachama kumudu kurejesha kwa wakati unaotakiwa. (iii) Hisa hutumika kama dhamana ya mkopo unaotolewa kwa mwanachama wa kikundi kidogo cha watu watano. Dhamana ya awali ni ya mkopaji mwenyewe (Primary Guarantor) na dhamana ya pili ni ya wanachama wenzake wanne (4) wa kikundi kidogo (Secondary Guarantors) Hii inamaanisha kuwa ili kuhakikisha kuwa mikopo yote inayotolewa kwa wanachama 5 wa kikundi kidogo inadhaminiwa kikamilifu mambo yafuatayo yanatakiwa kuzingatiwa: (a) Wanachama wa kikundi kidogo wasiruhusiwe kuchukua mkopo wakati mmoja. Tofauti ya mwezi mmoja hadi miezi miwilli ni kipindi kizuri kwa wastani wa watu wawili wawili kila awamu (b) Kunatakiwa pawepo na makubaliano maalumu baina ya mwanachama anayekopa na wale wanaomdhamini juu ya hatua zinazoweza kuchukuliwa na wadhamini endapo mdhaminiwa hatatimiza wajibu wa kulipa deni lake kwa uzembe (c) Mwanachama anayekopa kutoka kwenye benki ya kikundi anatakiwa kuchangia mfuko wa bima ya majanga itakayokubaliwa na kikundi kwa mfano kufariki kwa mkopaji, kuugua kwa muda mrefu na kupoteza uwezo wa kufanya kazi/ kulemaa kwa mkopaji kuunguliwa au kuibiwa mali za biashara ya mkopaji, ukame, nk Taratibu za utoaji na urejeshaji wa mikopo. Mikopo inayotolewa kwa wanachama wa VICOBA unatakiwa kurejeshwa na nyongeza (Interest) ndogo ambayo hutumika kwa kutunisha mfuko wa kikundi. Nyongeza hii hugawanywa kama faida kwa wanachama kwa kuzingatia kiwango cha hisa alizoweka kila mmoja. Mikopo ya mwanzo ambayo kwa kawaida huwa midogo kuliko mikopo inayofuata hutakiwa kulipwa kwa kipindi cha miezi 3 . Lengo ni kumwezesha mkopaji aweze kulipa haraka na kuchukua mkopo mkubwa pale hisa zake zinavyopanda ambao utamwezesha kumudu kuanzisha na kuendesha biashara madhubuti zaidi Mfumo wa VICOBA unamtaka mkopaji kurejesha mkopo aliokopa mwishoni mwa kipindi cha mkopo wake kwa awamu moja. Mkopaji anatakiwa kulipa sehemu ya nyongeza inayoiva kila ifikapo wiki ya mwisho ya mwezi. Sehemu ya mwisho hulipwa pamoja na mkopo Mfano: Endapo mwanachama atakapokopeshwa shilingi 100, 000.00 kwa nyongeza ya 10% (10,000.00) kwa kipindi cha miezi mitatu atarejesha kama ifuatavyo:- Mwezi wa 1 Mwezi wa 2 Mwezi wa 3 Jumla 3,400 3,300 3,300 100,000 110,000 Endapo mkopo wa thamani hiyo hiyo (Shilingi 100,000.00) utarejeshwa kwa kipindi cha miezi sita kwa gharama (nyongeza) ya asilimia ishirini 20% (20,000.00), marejesho yatakuwa kama ifuatavyo:- Mwezi wa 1 Mwezi wa 2 Mwezi wa 3 Mwezi wa 4 Mwezi wa 5 Mwezi wa 6 Jumla 3,400 3,400 3,300 3,300 3,300 3,300 100,000 120,000 Kwa kawaida mwanachama anayemaliza kurejesha mkopo wake vizuri anaruhhusiwa kuomba mkopo mwingine mara moja ili kufidia pengo la mtaji katika biashara yake. Ufuatiliaji na Uthibiti wa shughuli za vikundi vya VICOBA Makatibu wa vikundi vya VICOBA wanatakiwa kufuatilia mwenendo wa vikundi vyao na kuandaa taarifa za kila mwezi, miezi mitatu na taarifa za kila mwaka ambazo hujadiliwa na kupitishwa na mikutano mikuu ya vikundi vyao. Afisa (Mkufunzi) anatakiwa kutoa maelekezo na msaada wa kiufundi pale inapobidi na kuwajulisha wafadhali wa vikundi na wadau wengine juu ya maendeleo ya vikundi kadiri inavyotakiwa.