Sunday 10 November 2013

Umbeya, majungu, Kusengenya vinavuruga maendeleo

Wanakikundi wa Bahati VICOBA mnaaswa kuwa na ushirikiano na upendo katika kikundi chenu kama hamtaifuata salamu ya VICOBA basi mtabaki kunung'unika na kusengenya pembeni.  Wengi wenu hamna kazi za kufanya hivyo inawafanya kila muambiwalo la msingi mnahisi kuburuzwa ila tulizeni akili na mjue hamburuzwi ila hakuna maendeleo ya lelemama, kubalini fauateni maelekezo mnayopewa na wabunifu ili muje muone maendeleo.

Ndugu wanakikundi nayaongea haya kwa uchungu kwa kuwa naona kuna watu wasio waaminifu wanaanza kuvuruga kikundi, hakuna ubunifu, kuna majungu tu, kila tunalopanga mnalipeleka kwenye kundi linguine ni aibu sana mwanakikundi kunyenyekea kundi linguine kisa unapewa HISA na JAMII ni aibu sana kufuatilia fedha iliyo benki kama vile imeliwa hamtaendelea nawaambia.  Kama mnataka maendeleo fuateni mambo ya msingi na myafanyie kazi na si kukaa pembeni na kuanza kusimanga.

No comments:

Post a Comment