wanakikundi ni lazima tuelewe wiki ya 14 hii, tujifunze kazi za mkutano mkuu unaofanyika maramoja kwa maka ambao ndio unachagua viongozi.
Tujifunze jinsi ya kutatua migigoro itakapojitokeza
Tujifunze jinsi ya kuweka akiba
Jinsi ya kusimamia mikopo ya wanachama
Tujifunze jinsi ya namna ya kutunga kanuni na taratibu za vikundi na kuandika michanganuo rahisi ya biashara, ambayo ni msaada mkubwa katika kupanua wigo wa biashara zetu.
Kimsingi hatutakiwi kuvunja kikundi mwisho wa mwaka bali tuanzishe miradi ya vikundi ambayo itashirikisha wanachama wote.
Lazima kikundi chetu kitambulike serikali za mtaa pamoja na majirani
Lengo linguine ni kupeleka ujumbe kwa wananchi kwamba VICOBA kama wengine wanavyodhani kimakosa kuwa ni vikundi vya kufa na kuzikana. Wananchi wanakumbushwa kwamba hivi ni vikundi vya maendeleo ya uchumi.
Pia tujipange kualika vikundi mia tatu kuzindua kundi letu la BAHATI VICOBA
hapa tutapata kiasi cha shilingi milioni tisa (9,000,000/=) za kuzindilia kikundi
BAHATI VICOBA kina bahati kama jina lake, kuna THINKERS ila kuna watu wanataka kuharibu kundi kama tutaendelea kupanga mikakati ya kibwege nje ya mikutano na kulalama nje ya vikao halali kundi hili litakuwa HOPELESS na hakuna maendeleo yatakayofikiwa. wanajulikana waharibifu wa kikundi ila ipo siku watatajwa na wataachiwa kundi na wenye akili watatoka
No comments:
Post a Comment